2 Chronicles 32:27-29

27 aHezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani. 28Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi. 29 bAkajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ng’ombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.

Copyright information for SwhKC